Madereva wasitisha mgomo, mabasi ya mikoani yaanza kazi

By | 9:55 PM Leave a Comment
Hatimaye madereva wa mabasi na malori wameamua kusitisha mgomo leo baada ya Serikali kuwahakikishia kuwa inaandaa utaratibu mzuri wa kujibu na kushughulikia matatizo yao.
Mgomo huo ulioanza jana umesababisha usumbufu mkubwa kwa raia sehemu nyingi nchini Tanzania ambao walikuwa wamejiandaa kusafiri kuelekea katika mikoa mingine jana na leo kwa ajili ya shughuli zao mbalimbali zikiwemo za kibiashara na kijamii.
Taarifa zilizotufikia ni kwamba Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda akiwa na viongozi wengine wa Serikali walifika katika kituo cha mabasi yaendao mikoani cha ubungo na kuzungumza na madereva hao wakiwataka wasitishe mgomo wao na kuanza kazi kwani mambo yao Serikali inayafanyia kazi na hivi karibuni watajibiwa.
Kufuatia hali hiyo maderva hao walikubaliana na ombi hilo la Serikali baada ya kutokea kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe ambaye naye aliwasihi waache mgomo huo kwani Serikali itafanyia kazi maombi yao.
Ungana nasi baadaye kwa ajili ya tarifa zaidi.
xxxxxxx
Nchi yasimama: Madereva mabasi, malori wagoma sehemu kubwa ya Tanzania
Dar/mikoani. Nchi imesimama. Hii ndiyo sentensi inayofaa kuelezea tukio la jana la mgomo wa madereva nchini kote ambao kwa mara ya kwanza ulisababisha mabasi yote kutoka Dar es Salaam kwenda mikoani na nchi jirani kushindwa kuondoka.
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT), kushindwa kutoa huduma kwa sababu yoyote ile.
Tangu asubuhi hadi jioni, hakuna basi hata moja lililotoka wala kuingia katika kituo hicho hadi abiria walipoanza kukata tamaa na baadhi yao kuondoka na wengine kuanza kushinikiza kurejeshewa nauli.
Mgomo huo ambao ni mwendelezo wa ule uliofanyika Aprili 9, mwaka huu ulipewa uzito na madereva hao baada ya ahadi walizopewa na Serikali kutofanyiwa kazi kama ilivyoahidiwa na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka.

0 comments:

Post a Comment