Mgomo huo ulioanza jana umesababisha usumbufu
mkubwa kwa raia sehemu nyingi nchini Tanzania ambao walikuwa wamejiandaa
kusafiri kuelekea katika mikoa mingine jana na leo kwa ajili ya
shughuli zao mbalimbali zikiwemo za kibiashara na kijamii.
Taarifa zilizotufikia ni kwamba Mkuu wa Wilaya ya
Kinondoni Paul Makonda akiwa na viongozi wengine wa Serikali walifika
katika kituo cha mabasi yaendao mikoani cha ubungo na kuzungumza na
madereva hao wakiwataka wasitishe mgomo wao na kuanza kazi kwani mambo
yao Serikali inayafanyia kazi na hivi karibuni watajibiwa.
Kufuatia hali hiyo maderva hao walikubaliana na
ombi hilo la Serikali baada ya kutokea kwa Mwenyekiti wa Chama Cha
Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe ambaye naye aliwasihi waache mgomo
huo kwani Serikali itafanyia kazi maombi yao.
Ungana nasi baadaye kwa ajili ya tarifa zaidi.
xxxxxxx
Nchi yasimama: Madereva mabasi, malori wagoma sehemu kubwa ya Tanzania
Dar/mikoani. Nchi imesimama. Hii ndiyo sentensi
inayofaa kuelezea tukio la jana la mgomo wa madereva nchini kote ambao
kwa mara ya kwanza ulisababisha mabasi yote kutoka Dar es Salaam kwenda
mikoani na nchi jirani kushindwa kuondoka.
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT), kushindwa kutoa huduma kwa sababu yoyote ile.
Tangu asubuhi hadi jioni, hakuna basi hata moja
lililotoka wala kuingia katika kituo hicho hadi abiria walipoanza kukata
tamaa na baadhi yao kuondoka na wengine kuanza kushinikiza kurejeshewa
nauli.
Mgomo huo ambao ni mwendelezo wa ule uliofanyika
Aprili 9, mwaka huu ulipewa uzito na madereva hao baada ya ahadi
walizopewa na Serikali kutofanyiwa kazi kama ilivyoahidiwa na Waziri wa
Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka.
0 comments:
Post a Comment