The Latest

Dar es Salaam. Wakati madereva wa mabasi, malori na daladala wakiendelea na mgomo katika mikoa mbalimbali kuishinikiza Serikali kutekeleza madai yao, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameunda kamati ya kudumu ya kusimamia usafiri wa barabarani.
Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Samuel Sitta alisema jana kwamba kutokana na kutokea kwa mivutano baina ya wadau wa usafiri nchini mara kwa mara na kusababisha usumbufu kwa wananchi, Jumamosi iliyopita, Waziri Pinda aliunda tume itakayokuwa ikishughulikia matatizo yanayojitokeza.
“Lengo la kamati hii ni kuhakikisha kwamba wakati wote bila kusubiri migomo, kuwe na majadiliano shirikishi ya wadau wote ili kuyapatia ufumbuzi matatizo ya makundi mbalimbali katika usafiri wa barabarani,” alisema Sitta.
Aliwataja wanaounda kamati hiyo kuwa ni Katibu Mkuu, Wizara ya Uchukuzi, ambaye atakuwa mwenyekiti na katibu wake atakuwa Kamishna wa Polisi, Usalama Barabarani.
Wajumbe ni katibu mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani (Usimamizi wa Polisi na usalama barabarani) na katibu mkuu, Wizara ya Kazi na Ajira (Mikataba ya ajira kati ya Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa)/Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (Tatoa) na madereva).
Wengine ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Masuala ya sheria), naibu katibu mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, mkuu wa uratibu na Idara ya Maafa, mwenyekiti Taboa, mwenyekiti wa Tatoa
Mwenyekiti wa Chama cha Madereva wa Mabasi na Magari ya Mizigo, mwenyekiti wa chombo cha kusimamia haki za wasafiri na mkurugenzi wa Sumatra.
Kamati hiyo imetangazwa siku ambayo huduma za usafiri wa barabara zilisimama kutokana na mgomo wa madereva.
Mbagala mshikemshike
Mabomu ya machozi yaliyotupwa na polisi yalikuwa salama wananchi wenye magari binafsi baada ya kuwatimua mamia ya vijana waliokuwa wamefunga Barabara ya Kilwa eneo la Zakhiem na kusababisha msongamano mkubwa wa magari.
Vijana hao walifunga barabara na kuanza kushusha abiria kwenye magari binafsi na kuwalazimisha wenye magari hayo kuwapakia wanafunzi na kuwapeleka shule.
Shughuli hiyo hilo lililodumu kwa dakika 40 kuanzia saa 1.45 hadi saa 2.25 asubuhi. Vijana nao waliwashusha wafanyakazi wote waliokuwa kwenye basi la Kampuni ya Tanzania Road Haulage (TRH) waliokuwa wakienda kazini na kumlazimisha dereva kuwapakia wanafunzi na kuwapeleka shule.
Kufichwa ukweli wa ufahamu, utambuzi na ung’amuzi wa mambo muhimu katika maisha ndiyo msingi wa umaskini na matatizo yasiyopatiwa ufumbuzi.
Tunu hizo muhimu hujengwa na mifumo asili ya uumbwaji wa mwanadamu ambayo ni mila na utamaduni.
Elimu sahihi ni ile inayosaidia kukuza michepuo ya akili ambayo tayari binadamu amezaliwa nayo na hujengwa na mila, desturi na jadi.
Kwa bahati mbaya, tunafanya juhudi kubwa kuwekeza kwenye elimu bandia inayokaririsha watu nadharia bila kugusa michepuo ya akili.
Elimu ya vitabu na maandiko ya watu wa kale ambayo hayana muunganiko wala mafungamano na ujuzi wa au stadi za kufanikiwa kimaisha ndiyo masomo ya watoto wetu sasa.
Tunafundisha masomo badala ya ujuzi na maarifa. Tunawafundisha kushindwa kufikiri na kushindwa maisha.
Kubwa zaidi, utamaduni dhaifu wa wageni ndio unaochukuliwa kwa sasa kama elimu.
Mtu akizungumza, akicheza na kuvaa kama mzungu anashangiliwa na kupongezwa kuwa ameelimika hata kama hawezi hata kushona kifungo cha shati lake.
Tuna maprofesa waliosomea uhandisi wa maji, wanazungumza Kiingereza kizuri na kuvaa suti kama wazungu, lakini nyumbani wanashindwa kuvuna maji ya mvua.
Viashiria bainifu vya elimu sahihi inayokuza vipawa na michepuo ya akili ni kuwa na watu wanaojitambua, wanaovumbua majibu ya matatizo yao, wanaobuni, wanaochangamkia fursa na kuwa na dira na malengo sahihi ya maisha.
Kufahamu upo duniani kwa ajili ya nini, ili ufanye nini, kwa manufaa ya nani na wakati gani. Ndiyo nguvu ya elimu sahihi.
Tofauti na elimu bandia ambayo inakaririsha nadharia ombwe kwa watu na kuviza vipaji vyao.
Hatimaye madereva wa mabasi na malori wameamua kusitisha mgomo leo baada ya Serikali kuwahakikishia kuwa inaandaa utaratibu mzuri wa kujibu na kushughulikia matatizo yao.
Mgomo huo ulioanza jana umesababisha usumbufu mkubwa kwa raia sehemu nyingi nchini Tanzania ambao walikuwa wamejiandaa kusafiri kuelekea katika mikoa mingine jana na leo kwa ajili ya shughuli zao mbalimbali zikiwemo za kibiashara na kijamii.
Taarifa zilizotufikia ni kwamba Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda akiwa na viongozi wengine wa Serikali walifika katika kituo cha mabasi yaendao mikoani cha ubungo na kuzungumza na madereva hao wakiwataka wasitishe mgomo wao na kuanza kazi kwani mambo yao Serikali inayafanyia kazi na hivi karibuni watajibiwa.
Kufuatia hali hiyo maderva hao walikubaliana na ombi hilo la Serikali baada ya kutokea kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe ambaye naye aliwasihi waache mgomo huo kwani Serikali itafanyia kazi maombi yao.
Ungana nasi baadaye kwa ajili ya tarifa zaidi.
xxxxxxx
Nchi yasimama: Madereva mabasi, malori wagoma sehemu kubwa ya Tanzania
Dar/mikoani. Nchi imesimama. Hii ndiyo sentensi inayofaa kuelezea tukio la jana la mgomo wa madereva nchini kote ambao kwa mara ya kwanza ulisababisha mabasi yote kutoka Dar es Salaam kwenda mikoani na nchi jirani kushindwa kuondoka.
Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT), kushindwa kutoa huduma kwa sababu yoyote ile.
Tangu asubuhi hadi jioni, hakuna basi hata moja lililotoka wala kuingia katika kituo hicho hadi abiria walipoanza kukata tamaa na baadhi yao kuondoka na wengine kuanza kushinikiza kurejeshewa nauli.
Mgomo huo ambao ni mwendelezo wa ule uliofanyika Aprili 9, mwaka huu ulipewa uzito na madereva hao baada ya ahadi walizopewa na Serikali kutofanyiwa kazi kama ilivyoahidiwa na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka.